Monday, April 22, 2019

SALA YA MSAFIRI 3/4

*KUKUSANYA KWA KUCHELEWESHA:*

Kwa Maana Kuisali Adhuhuri na Laasiri ndani ya Wakati wa Laasiri
Au
Kuisali Magharibi na Isha Ndani ya Wakati wa Isha.

*SHARTI ZA KUCHANGANYA KWA KUCHELEWESHA NI 2:*

*1.* Kutia Nia ya Kuchelewesha katika Wakati wa Sala ya Mwanzo ile hali bado Wakati wa Sala
hiyo haujesha.
*2.* Udumu Udhuru Mpaka kukamilika kwa Wakati wa Sala ya pili.

*KUPUNGUZA SALA*
Msafiri anayoruhusa ya kusali
*A.* Adhuhuri Rakaa 2
*B.* Laasiri Rakaa 2
*C.* Isha Rakaa 2.

*SHARTI ZA KUPUNGUZA SALA NI 11:*

*1.* Iwe ni Kwa Sala za Faradhi za Rakaa Nne Nne tu.
*2.* Ukusudie (Uijue) Sehemu Unayokwenda.
*3.* Iwe Safari ni ya Halali.
*4.* Safari iwe ni kwa Malengo Yaliyo sahihi (Malengo yanayokubalika Kisheria)
*5.* Safari iwe na Umbali wa Kilomita 82.
*6.* Iwe baada ya Kuvuka (Kuuwacha) Mji.
*7.* Uwe na Elimu ya Kupunguza Sala kisheria.
*8.* Idumu Safari mpaka kutimia kwa Sala zote mbili.
*9.* Kutia Nia ya Kupunguza Sala wakati wa Kuhirimia.
*10.* Kujiempusha na yale yote yanayokwenda kinyume na Nia ya Kupunguza Sala.
*11.* Usimfuate Mtu anaekamilisha Sala.

*.........................................................*
*3/4*

No comments:

Post a Comment

 
back to top