*السلام عليكم ورحمة الله وبركاته*
*صلاة المسافر*
*SALA YA MSAFIRI*
*قال رسول الله صلى الله عليه وسلم "السفر قطعة من العذاب"*
*Amesema Mtume S.A.W "Safari ni sehemu ya Adhabu"*
��Msafiri anaruhusiwa Kusali Sala Kwa kutumia Moja ya Hali zifuatazo;
*1.* *Kuchanganya (Kukusanya pamoja) Baina ya Sala mbili.*
Yaani Mfano Sala ya Adhuhuri na Laasir akazisali ndani ya Wakati mmoja
*2.* *Kuacha kukusanya (Kila Sala Akasali kwa Wakati wake).*
*3.* *Kupunguza Sala*
kwa Maana Sala za Rakaa Nne akazisali kwa Rakaa mbili mbili.
*4.* *Kutimiza .* Kwa Maana Sala zote kuzisali kwa Ukamilifu wa Rakaa Zake.
*KUKUSANYA SALA NA UTARATIBU WAKE:*
Unaweza kukusanya
*A.* Adhuhuri na Laasiri
*B.* Magharibi na Isha.
*Pia Kukusanya Sala Kuna Hali Mbili*
*1.* Kukusanya Kwa Kutanguliza.
*2.* Kukusanya kwa Kuchelewesha.
*SABABU ZA KUKUSANYA SALA NI 3*
*1.* *Safari ;* Kutanguliza na Kuchelewesha.
*2.* *Mvua;* Kutanguliza tu.
*3.* *Ugonjwa(Kuumwa);* Kutanguliza na Kuchelewesha.
*.........................................................*
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment